Dkt. Chegeni, Lawrence Masha watiwa mbaroni jijini Mbeya
Kamanda wa Polisi wa mkoani humo, Ulrich Matei amesema wawili hao walikamatwa jana, kuhojiwa na kuachiwa kwa dhamana.
Amesema polisi walipata taarifa kutoka katika ubalozi wa Ujerumani kwamba kuna mabaunsa 20 wamevamia nyumba ya mwekezaji huyo mwenye mashamba ya parachichi.
“Masha na Chegeni walikuwa wanatimiza wajibu wao kwa mujibu wa Mahakama ya kumuondoa mwekezaji huyo katika eneo lile,” amesema Matei.
“Hata hivyo hawakufuata utaratibu ikiwemo kumpa taarifa mhusika na haikuwa siku ya kazi. Kama yule Chegeni ni mbunge angetumia utaratibu hata kupitia kwa mkuu wa mkoa kuliko kufanya kama vile.
Amebainisha kuwa walipopata taarifa kutoka ubalozi wa Ujerumani ziliwashtua kwa sababu Tanzania ni nchi ya amani.
Kwa mujibu wa Kamanda Matei, polisi walipofika eneo hilo walikuta baadhi ya vitu vimeharibiwa huku mwekezaji huyo ambaye ni mwanamke akijeruhiwa sehemu mbalimbali mwilini.
Amesema polisi walipata taarifa kutoka katika ubalozi wa Ujerumani kwamba kuna mabaunsa 20 wamevamia nyumba ya mwekezaji huyo mwenye mashamba ya parachichi.
“Masha na Chegeni walikuwa wanatimiza wajibu wao kwa mujibu wa Mahakama ya kumuondoa mwekezaji huyo katika eneo lile,” amesema Matei.
“Hata hivyo hawakufuata utaratibu ikiwemo kumpa taarifa mhusika na haikuwa siku ya kazi. Kama yule Chegeni ni mbunge angetumia utaratibu hata kupitia kwa mkuu wa mkoa kuliko kufanya kama vile.
Amebainisha kuwa walipopata taarifa kutoka ubalozi wa Ujerumani ziliwashtua kwa sababu Tanzania ni nchi ya amani.
Kwa mujibu wa Kamanda Matei, polisi walipofika eneo hilo walikuta baadhi ya vitu vimeharibiwa huku mwekezaji huyo ambaye ni mwanamke akijeruhiwa sehemu mbalimbali mwilini.
Dkt. Chegeni, Lawrence Masha watiwa mbaroni jijini Mbeya
Reviewed by Zero Degree
on
10/28/2018 12:20:00 PM
Rating:
Reviewed by Zero Degree
on
10/28/2018 12:20:00 PM
Rating:
