Orodha ya wachezaji 11 wenye umri mkubwa zaidi barani Ulaya
Petr Cech akiwa na Gianluigi Buffon |
Badala ya kustaafu, golikipa huyo kutoka Italia aliondoka Juventus kwenda Paris Saint-Germain kuendeleza msako wa taji la Ligi ya Mabingwa kabla hajaachana na kazi yake ya kulinda goli.
Ana wachezaji kama nyota wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar na chipukizi mwenye kipaji cha kipekee Kylian Mbappe wa kumsaidia kufanya hivyo na bado anaendelea kuonyesha umahiri wake pale anaposimama golini.
Hata hivyo, Buffon hayuko peke yake. Wapo wakongwe wengi ambao bado wanaendelea kusaka rekodi kwenye soka.
Zero Degree imejaribu kupitia takwimu kutoka tovuti ya WhoScored.com na kuwekea majina ya wachezaji 11 wenye umri miaka 33 na kuendelea kutoka ligi tano kubwa barani Ulaya.
11. Gianluigi Buffon (Paris Saint-Germain)
10. Petr Cech (Arsenal)
9. Rune Jarstein (Hertha Berlin)
8. Giorgio Chiellini (Juventus)
7. Thiago Silva (Paris Saint-Germain)
6. Jose Holebas (Watford)
5. Filipe Luis (Atletico Madrid)
4. Sol Bamba (Cardiff City)
3. Pablo Zabaleta (West Ham)
2. Fernandinho (Manchester City),
1. Cristiano Ronaldo (Juventus)
Orodha hiyo ni kwa mujibu wa takwimu za WhoSocored.com, lakini haimanishi kwamba hao ndio wachezji pekee wenye umri mkubwa zaidi barani Ulaya.
Orodha ya wachezaji 11 wenye umri mkubwa zaidi barani Ulaya
Reviewed by Zero Degree
on
10/18/2018 08:40:00 AM
Rating: