Ajali ya basi yaua wawili Lushoto
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda waPolisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, amesema basi hilo lilikua likisafiri kutoka Tanga kwenda wilayani Lushoto.
Kamanda Bukombe amebainisha chanzo cha ajali hiyo ni utelezi uliotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika eneo hilo.
“Majeruhi sita kati ya 21 hali zao ni mbaya na wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa matibabu zaidi,” amesema.
Ajali ya basi yaua wawili Lushoto
Reviewed by Zero Degree
on
12/12/2018 07:35:00 AM
Rating: