Loading...

FA: Manchester United kukipiga dhidi ya Mabingwa watetezi Chelsea


Mabingwa watetezi wa kombe la FA, Chelsea, wataminyana na mabingwa mara 12 wa kombe hilo, Manchester United, katika mzunguko wa tano wa michuano hiyo.

Mechi ya miamba hiyo itakuwa ni marudio ya fainali ya mwaka jana ambapo Chelsea waliibuka na ushindi.

Timu ya Ligi Daraja la Pili ya Newport County wanaweza kuminyana na mabingwa wa Ligi ya Premia Manchester City iwapo watawang'oa Middlesbrough katika mechi yao ya marudiano.

Timu ya Ligi Daraka la Kwanza Doncaster Rovers wamenuwia kuwang'oa Crystal Palace iliyopo kwenye Ligi ya Premia baada ya kutoka sare mchezo wao wa kwanza wa mzunguko wa nne.

Michezo ya raundi ya tano ya michuano ya FA itapigwa kati ya tarehe 15 na 18 ya mwezi Februari.

Ratiba kamili ya raundi ya tano ya FA:
  • Bristol City Vs Shrewsbury Town/Wolverhampton Wanderers
  • AFC Wimbledon Vs Millwall
  • Doncaster Rovers Vs Crystal Palace
  • Middlesbrough/Newport County Vs Manchester City
  • Chelsea Vs Manchester United
  • Swansea v Barnet or Brentford
  • Portsmouth/Queens Park Rangers Vs Watford
  • Brighton & Hove Albion/West Bromwich Albion Vs Derby County
FA: Manchester United kukipiga dhidi ya Mabingwa watetezi Chelsea FA: Manchester United kukipiga dhidi ya Mabingwa watetezi Chelsea Reviewed by Zero Degree on 1/29/2019 08:35:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.