Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano Septemba 25, 2019


Manchester United inapania kumsajili mshambulizi wa Juventus wa miaka 33 Mcroatia Mario Mandzukic na kiungo wa kimataifa wa Ufaransa na Barcelona Ousmane Dembele, 22, Januari Mwakani. (The Independent)

Maafisa wa matibabu wa mshambuliaji wa Newcastle na England Andy Carroll, 30, wanahofia mchezaji huyo huenda isiingie uwanjani hadi baada ya Krismasi japo anaendelea kupata nafuu kufuatia jaraha la mguu alilopata. (Telegraph)

Klabu ya Manchester United inafuatilia mchezo wa kiungo wa kati wa Italia wa miaka 19 Sandro Tonali atashiriki mechi ya Brescia dhidi ya Juventus siku ya Jumanne. (Mail)

Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesema meneja wa sasa wa Rangers na nahodha wa zamani wa Reds Steven Gerrard ndiye atakayemrithi atakapiamua kuondoka Anfield. (FourFourTwo)

Mshambuliaji wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, bado anataka kuondoka Crystal Palace na anapania kushinikiza uhamisho dirisha la uhamisho wa wachezaji litakapofunguliwa tena mwezi Januari Mwakani. (Calciomercato)

Sevilla iko tayari kumuachilia kiungo wa kati wa Ureno Rony Lopes mwezi January, huku Newcastle ikimfuatilia mkufunzi huyo wa zamani wa Manchester City wa miaka 23. (Gol Digita)

Mshambuliaji wa zamani wa Celtic na Manchester United Henrik Larsson huenda akapewa wadhifa wa Southend, kutokana na hali ngumu ya kiuhchumi inayomkabili na ukosefu wa tajiriba ya ukufunzi wa vilabu vya Uingereza ambao umekua changamoto kwake . (Sky Sports)

Mauricio Pochettino

Meneja wa Tottenham, Mauricio Pochettino amegusia kuwa klabu hiyo itakuwa na shughuli nyingi mwezi Januari dirisha la uhamisho wa wachezaji litakapofunguliwa huku wakijiandaa kwa mchuano wa kombe Carabao Cup dhidi ya Colchester inayoshiriki soka ya daraja la pili. (Express)

Mkurugenzi mkuu wa Arsenal Vinai Venkatesham amesema kuwa klabu hiyo huenda isajili wachezaji wapya mwezi Januari wakati wa uhamisho wa wachezaji. (Standard)

Meneja wa Newcastle Steve Bruce ana mpango wa kumtoa katika kikosi cha kwanza mshambuliaji wa Paraguay forward Miguel Almiron aliyejiunga na klabu hiyo mwezi Januari kwa £20m. (Star)

Chanzo: BBC
Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano Septemba 25, 2019 Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano Septemba 25, 2019 Reviewed by Zero Degree on 9/25/2019 08:35:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.