Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 29 Mei, 2024


Nia ya Xavi ya kumuuza mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski mwenye umri wa miaka 35 msimu huu ilikuwa sababu kuu ya Mhispania huyo kufukuzwa kazi Barcelona mwezi huu.

Barcelona huenda wakamrejesha Nou Camp kwa mara ya pili mshambuliaji wa Ureno Joao Felix kutoka Atletico Madrid. (Sport)

Klabu kadhaa za ligi kuu ya Saudia (Saudi Pro), ikiwemo Al Nassr, Al Ahli na Al Qasidiya, zinawania kumsajili kiungo wa kati wa timu ya taifa ya Brazil Casemiro, 32, kutoka Manchester United msimu huu. (Goal)

West Ham wamefikia mkataba wa pauni milioni 15 na Flamengo kumnunua mlinzi wa Brazil Fabricio Bruno, 28. (Guardian)

Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Muingereza Mason Greenwood anataka kurejea katika klabu ya Getafe ya Uhispania msimu ujao baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 hivi majuzi kucheza mechi yake ya mwisho kama mchezaji wa mkopo katika klabu hiyo ya La Liga. (TEAMtalk)

Aston Villa na Crystal Palace wanatazamia kumnunua beki wa Gent Muingereza Archie Brown, 22. (Mirror)

Newcastle wanashinikiza kupata jibu kuhusu uwezekano wa kumnunua beki wa Uingereza Tosin Adarabioyo, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 akitarajiwa kuondoka Fulham msimu huu wa joto mkataba wake utakapomalizika. (Talksport)

Liverpool wameweka thamani ya pauni milioni 20 kwa mlinzi wa Uholanzi Sepp van den Berg, 22, ambaye ananyatiwa na klabu za Brentford, Southampton na Wolfsburg baada ya kung'aa alipokuwa Mainz kwa mkopo. (Athletic)

Napoli hawana nia ya kumuuza winga wa Georgia Khvicha Kvaratskhelia, 23, kwa Paris St-Germain, huku Antonio Conte akitarajiwa kuwa kocha wao mkuu mpya. (Corriere dello Sport)

Mshambuliaji wa Real Madrid wa Brazil Rodrygo, 23, ametilia shaka mustakabali wake katika klabu hiyo

Mshambuliaji wa Real Madrid wa Brazil Rodrygo, 23, ametilia shaka mustakabali wake katika klabu hiyo, na hivyo kuongeza uwezekano wa kuhamia Liverpool. (Mundo Deportivo)

Kinyang'anyiro cha kumsaka mshambuliaji wa RB Leipzig na Uhispania Dani Olmo kimeshika kasi, huku Barcelona, ​​Manchester United, Manchester City, Liverpool na Bayern Munich zikimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Mundo Deportivo)

Klabu ya Southampton wanawania saini ya winga wa Sunderland Muingereza Jack Clarke, 23. (Telegraph)

Inter Milan wanavutiwa na beki Mwingereza Aaron Wan-Bissaka, 26, ambaye Manchester United imeweka thamani yake kuwa euro 12m (£10.2m). (Tuttomercatoweb)

Arsenal na kocha Mikel Arteta wapo kwenye mazungumzo kuhusu mkataba mpya wa kudumu katika klabu hiyo. (Football Insider)
Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 29 Mei, 2024 Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 29 Mei, 2024 Reviewed by Zero Degree on 5/29/2024 08:51:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.