Loading...

TCRA kuzifutia leseni kampuni za simu zisizojisajili katika soko la hisa [DSE].

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA),James Kilaba.
Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA), James Kilaba amesema makampuni yote ya simu yanayotoa huduma za mawasiliano na yaliyotakiwa kujisajili kwenye soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) ili kuuza asilimia 25 ya hisa zake na hayajafanya hivyo yataadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mhandisi Kilaba amesema kwa sasa mamlaka hiyo inasubiri taarifa kutoka kwenye mamlaka ya soko la mitaji na dhamana kufahamu idadi ya kampuni ambazo hazijajiorodhesha na adhabu yake kisheria ni kufutiwa leseni ya kutoa huduma.

“Kazi yetu ni moja tu kutekeleza sheria iliyopo inayohitaji wao kuwa wamejisajili, kwahiyo kwa ufupi nitaweka wazi kwamba, sheria ya nchi imepitishwa na bunge letu tukufu, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwahiyo na sisi kama watekelezaji tuko tayari kuitekeleza sheria hii ,sheria inatamka hivi anaweza kufutiwa leseni au leseni inaweza ikasitishwa,” alisema Kilaba.

ZeroDegree.
TCRA kuzifutia leseni kampuni za simu zisizojisajili katika soko la hisa [DSE]. TCRA kuzifutia leseni kampuni za simu zisizojisajili katika soko la hisa [DSE]. Reviewed by Zero Degree on 1/04/2017 05:18:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.