Loading...

Beki wa Cameroon, Nicolas Nkoulou atangaza kuachana na timu yake ya taifa

Mabingwa wa Afrika, Cameroon wamepata pigo baada ya beki wake Nicolas Nkoulou kutangaza kupumzika kuichezea timu hiyo ya taifa.

Beki huyo mwenye miakae 26, alifunga bao katika mchezo wa fainali wakati wakichapa Misri kwa mabao 2-1.

Nkoulou ameichezea Indomitable Lions mechi 74, pia alishakuwa nahodha wa timu hiyo .

"Baada ya kutwaa ubingwa wa Mataifa ya Afrika, naona wakati wangu kuichezea timu ya taifa umefika mwisho," aliumbia mtandao wa Foot Mercato.

"Tangu nilipoanza kucheza soka, wakati wote nimekuwa nikijitoa kwa timu yangu ya taifa. Malengo kila siku yaendelea na hiyo ndiyo hali yangu ilivyo.

"Uamuzi huu ni mgumu kuchukua nimeangalia faida na hasara kabla ya kuchuamua uamuzi huu."


Beki wa Cameroon, Nicolas Nkoulou atangaza kuachana na timu yake ya taifa Beki wa Cameroon, Nicolas Nkoulou atangaza kuachana na timu yake ya taifa Reviewed by Zero Degree on 3/08/2017 12:16:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.