Loading...

Kinyesi cha binadamu chakutwa kwenye Makopo ya soda ya Coca Cola

Polisi wameanzisha uchunguzi wa kile kilichoonekana kuwa kinyesi cha binadamnu, kupatikana kwenye makopo ya soda iliyowasilishwa kwenye kiwanda cha Coca Cola huko Ireland kaskazini.

Shughuli za usiku katika kiwanda cha Lisburn zilivurugwa wiki iliyopita wakati mashine zilipokwama.

Kampuni hiyo ilisema kuwa kisa hicho hakikuathiri vinywaji vyovyote ambavyo kwa sasa viko sokoni.

Polisi wanachunguza ripoti kuwa mikebe mingi huenda ilichafuka.


Kiwanda cha Coca Cola cha Knockmore, Lisburn
Msemaji wa Coca-Cola amesema kuwa kampuni hiyo ilikuwa ikifahamu kisa hicho cha makopo matupu katika kiwanda cha Knockmore.

"Tatizo hilo lilitambuliwa mara moja na bidhaa zote zilizoathirika kuzuiwa na haziwezi kuuzwa. Hiki ni kisa kilicho kando na hakiathiri biddaa zozote zilizo sokoni."msemaji wa Coca Coa alisema.
Kinyesi cha binadamu chakutwa kwenye Makopo ya soda ya Coca Cola Kinyesi cha binadamu  chakutwa kwenye Makopo ya soda ya Coca Cola Reviewed by Zero Degree on 3/29/2017 12:30:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.