Loading...

Pirlo kujiunga na Ligi Kuu ya Uingereza??

Kulingana na taarifa za vyombo vya habari, Conte yuko katika mchakato wa kumsaka kocha mpya lengo lake kubwa likiwa ni kumnasa Andrea Pirlo.

Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kocha wa zamani wa 'The Blues' Ray Wilkins.

Tangu Steve Holland alipojiunga na Uingereza mwaka jana, inasemekana Conte amekua na nia ya kuijaza nafasi yake na mtu mwingine ili kusaidiana katika shughuli za kila siku.

Aliyekuwa kocha wa 'The Blues', Ray Wilkins amedai kuwa muitaliano huyo mwenye umri wa miaka 47 ameweka macho yake kwa nguli wa soka toka Italia, Andrea Pirlo.

"Pirlo, ni muitaliano anayeweza kuongea Kiingereza na kuna uwezekano mkubwa akawasili kesho," Wilkins aliiambia talkSPORT.

"Najua kwa hakika yeye [Pirlo] amekuwa akionekana Stamford Bridge mara kadhaa msimu huu.

"Nina uhakika anataka kumleta mkongwe huyo - ambaye aliweza kuwa naye kama kocha wake hadi pale alipofikisha umri wa miaka 34 wakati akiwa na Juventus."

Pirlo alimmwagia sifa nyingi kocha wake wa zamani mwezi uliopita katika mahojiano na ESPN .

"Kwa upande wangu, Conte ni kocha bora," alisema Pirlo..

"Yeye ni 'genius'. Anafanya kazi kila siku, kila wakati unaohusu soka, timu, kila kidogo chochote kuhusiana na kazi yake. "
Pirlo kujiunga na Ligi Kuu ya Uingereza?? Pirlo kujiunga na Ligi Kuu ya Uingereza?? Reviewed by Zero Degree on 4/05/2017 03:45:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.