Loading...

Cristiano Ronaldo ataja wachezaji wanaoweza kurithi mikoba yake

Cristiano Ronaldo amechagua wachezaji anahohisi watapita katika nyayo zake na kushinda tuzo ya Mchezaji bora wa kiume wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.


Nyota huyo wa Real Madrid alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa kiume kwa mwaka 2017 siku ya Alhamisi.

Hazard alicheza wakati Chelsea(Under-23) inapoteza kwa kukubali kichapo cha goli 3-0 dhidi ya Everton jana Ijumaa, lakini kwa sasa anaonekana yuko fiti hata hivyo alikuwa na mchango mkubwa wakati Chelsea ikichukua ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu uliopita.


Ronaldo mwenye umri wa miaka 31, anahisi Hazard ni mmoja wa wachezaji ambao wanaweza kuchukua nafasi yake, pamoja na wengine kama Marcus Rashford, Neymar na chipukizi wengine wanaoonyesha kiwango cha juu Ulaya.

“Ninawaona wachezaji kadhaa wenye kiwango cha juu: Kama Asensio, Mbappe, Neymar, Dembele, Hazard, Rashford … na kadhilika,” 'Daily Mail' wanamripoti Ronaldo akiyasema hayo.

“Katika kizazi kijacho kuna kama wachezaji kumi ivi wenye kiwango cha juu zaidi.”
Cristiano Ronaldo ataja wachezaji wanaoweza kurithi mikoba yake Cristiano Ronaldo ataja wachezaji wanaoweza kurithi mikoba yake Reviewed by Zero Degree on 8/26/2017 05:10:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.