Loading...

UN yaiwekea Korea Kaskazini vikwazo vipya


Baraza la usalama la umoja wa mataifa limepiga kura kwa kauli moja kuiwekea vikwazo Korea Kaskazini kama adhabu ya kufanyia majaribio zana zake za nuklia.

Vikwazo hivyo vinalenga kuhujumu uwezo wa Pyongyang kufadhili na kutoa nafasi kwa mpango wake wa nuklya.

Vikwazo hivyo vilevile vinatoa masharti kwa biashara ya kununua mafuta mbali na kupiga marufuku uuzaji wa nguo katika mataifa ya kigeni.

Maamuzi hayo ya baraza la usalama la umoja wa mataifa yaliungwa mkono kwa wingi wa kura baada ya Marekani kuondoa mpango wake wa kutaka uungwaji mkono kutoka Urusi na China

Korea Kusini inasema kuwa kwa kuhujumu amani Korea Ksakzini itaewekewa vikwazo zaidi vya kimataifa.

Balozi wa China katika Umoja wa kimataifa Liu Jieyi ameitaka Korea Kaskazini kuchukua kwa umuhimu mkubwa matarajio ya jamii ya kimataifa na kuharibu mpango wa kinyuklia.

Kura hiyo ilipitishwa baada ya washirika wa Pyongyang ikiwemo Urusi na China kuilazimu Marekani kupunguza vikwazo hivyo.

Vikwazo hivyo ambavyo vilipitishwa katika baraa hilo la umoja wa mataifa vilipingwa na Korea Kaskazini.

Taarifa ya chombo cha habari cha Korea Kaskazini KNCA imeonya kwamba iwapo Marekani itasisitiza vikwazo vikali dhidi ya taifa hilo Korea Kasakzini itahakikisha kuwa Marekani inagharamikia hilo.

Hatua ya Marekani ya kutaka Korea Kaskazini kuwekewa vikwazo vya ununuzi wa mafuta kutoka nje ilionekana kama hatua itakayoliyumbisha taifa hilo.
Mpango wa kupiga tanji mali ya taifa hilo mbali na marufuku ya kusafiri ya rais Kim Jong Un uliondolewa.

Balozi wa Marekani katika umoja wa mataifa Nikki Haley aliambaia baraza la usalama la umoja wa mataifa baada ya kura hiyo kwamba hatufurahii kuiongezea vikwazo Korea kaskazini. hatutaki vita.

Msemaji wa rais wa Korea Kaskazini alisema siku ya Jumanne :Korea Kaskazini inahitaji kujua kwamba hujuma yoyote dhidi ya amani ya kimataifa itapelekea taifa hilo kuwekewa vikazo zaidi.
UN yaiwekea Korea Kaskazini vikwazo vipya UN yaiwekea Korea Kaskazini vikwazo vipya Reviewed by Zero Degree on 9/12/2017 09:27:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.