Loading...

Tenga ateuliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa BMT

Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Tanzania(TFF), Leodgar Tenga
Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Tanzania(TFF), Leodgar Tenga ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Waziri wa Habari Utamaduni wa Michezo, Harison Mwakyembe amethibitisha hilo kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari leo Ijumaa mchana.

Mwakyembe pia amewateua wajumbe sita wa BMT ambao ni Profesa Mkumbwa Mtambo, Beatrice Singano, Kanali Mstaafu Juma Ikangaa,Joseph Ndumbaro,Rehema Madenge na Salmini Kaniki.

Awali, BMT ilikuwa chini ya Dioniz Malinzi ambae uteuzi wake ulisitishwa na Wizara baada ya kutoridhika na utendaji wake.


Tenga ateuliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa BMT Tenga ateuliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa BMT Reviewed by Zero Degree on 2/09/2018 04:45:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.