Loading...

Kauli ya Pro. Jay baada ya viongozi Chadema kuwekwa rumande


Msanii Mkongwe wa Bongo fleva na Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule(Professor Jay) baada ya viongozi wao kunyimwa dhamana na kupelekwa rumande siku ya jana mbunge huyo ameandika mambo hayo yana mwisho.

“Yana mwisho Haya… Giza linapozidi kuwa Totoro jua kuwa karibu kunapambazuka.. TIME WILL TELL,” ameandika Professor Jay kwenye mitandao yake ya kijamii.

Viongozi hao baada ya kufika Mahakamani hapo walisomewa mashtaka nane katika Mahakama hiyo ikiwemo kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha Mwanafunzi wa Chuo cha NIT, Akwilina Akwiline Bafta.

Katika mashtaka hayo, Mh. Freeman Mbowe anakabiliwa na mashtaka saba ambayo ni kufanya mkusanyiko usio halali, maandamano, kuhamasisha chuki na uchochezi wa Uhasi.
Kauli ya Pro. Jay baada ya viongozi Chadema kuwekwa rumande Kauli ya Pro. Jay baada ya viongozi Chadema kuwekwa rumande Reviewed by Zero Degree on 3/28/2018 11:33:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.