Loading...

Aliyempa mimba dada yake ahukumiwa miaka 30 jela


Mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina la Charles Abel (24) Mkazi wa kijiji cha Usagara Mkoani Mwanza, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, kwa makosa mawili ya kubaka na kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la saba ambaye ni mtoto wa baba yake mkubwa.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Misungwi, Erick Marley akisoma hukumu hiyo juzi alisema amechukua maamuzi hayo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Akitoa ushahidi mahakamani hapo, Mwanafunzi huyo aliiambia mahakama kwamba mnamo Juni 6 saa 1:30 usiku akiwa chumbani kwake aliingiliwa na kubakwa na kaka yake (Charles Abel) ambaye ni mtoto wa baba yake mkubwa.

Mshtakiwa akijijitetea mahakamani hapo, aliomba kupunguziwa adhabu akidai kuwa hawezi kufanya mapenzi na dada yake na kwamba ametengenezewa kesi hiyo .

Hakimu Marley alisema Mahakama inamhukumu mshtakiwa kwa kosa la kwanza la ubakaji kifungo miaka 30 jela na kwamba, shtaka la pili la kumpa mimba mwanafunzi atatumikia miaka 30 jela, huku akieleza kuwa sababu adhabu zote zinakwenda pamoja atatumikia miaka 30 tu badala ya miaka 60.

Source: Mwananchi
Aliyempa mimba dada yake ahukumiwa miaka 30 jela Aliyempa mimba dada yake ahukumiwa miaka 30 jela Reviewed by Zero Degree on 11/02/2018 12:31:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.