Zitto aachiwa kwa dhamana
Zitto anatuhumiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu mauaji ya baadhi ya askari polisi na wananchi katika kijiji cha Mpeta, wilayani Uvinza mkoa wa Kigoma ambapo mara baada ya kukamatwa alipelekwa kwenye Kituo cha polisi cha Oysterbay, kabla ya kuhamishiwa polisi kati na baadaye kulazwa kwenye kituo cha polisi Mburahati.
Kabla ya kukamatwa na Polisi, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kigoma, Martin Ottieno, alimtaka Zitto kuwasilisha alichokiita, “vielelezo vya madai yake,” kuwa watu zaidi ya 100 wameuwa katika eneo la Uvinza.
Zitto ambaye ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT- Wazalendo, aliwaambia waandishi wa habari wiki iliyopita kuwa wananchi zaidi ya 100 wamepoteza maisha katika vurugu zilizoibuka kufuatia mgogoro wa ardhi wilayani Uvinza.
Zitto aachiwa kwa dhamana
Reviewed by Zero Degree
on
11/02/2018 03:05:00 PM
Rating: