Amber Rutty, James Delicious wafikishwa mahakamani
Amber Ruty na mpenzi wake wanatuhumiwa kufanya ngono kinyume cha maumbile na kusambaza picha/video za kwenye mitandao ya kijamii na James Delicious anatuhumiwa kujihusisha na vitendo vya mapenzi ya jinsia moja (ushoga).
Amber Rutty ambaye amefikishwa Mahakamani hapo akiwa anachechemea na kushindwa kukaa hadi alipopatiwa huduma ya kwanza na askari, pamoja na mpenzi wake wamesomewa mashtaka matatu, moja la kufanya mapenzi kinyume na maumbile, shtaka la pili ni kurekodi video za ngono na shtaka la tatu ni kusababisha kusambaa kwa picha na video za ngono kupitia mtandao wa WhatsApp.
Amber Rutty ambaye amefikishwa Mahakamani hapo akiwa anachechemea na kushindwa kukaa hadi alipopatiwa huduma ya kwanza na askari, pamoja na mpenzi wake wamesomewa mashtaka matatu, moja la kufanya mapenzi kinyume na maumbile, shtaka la pili ni kurekodi video za ngono na shtaka la tatu ni kusababisha kusambaa kwa picha na video za ngono kupitia mtandao wa WhatsApp.
“Hata hivyo watuhumiwa wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kukidhi masharti ya dhamana ambayo walitakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini bondi ya Tsh. Milioni 15 kila mmoja.
Wakati huo huo kijana anayejulikana kwa jina la James delicious naye amepandishwa mahakamani na kusomewa shtaka moja la kusambaza video za ngono mtandaoni, ambapo amekana shtaka hilo.
Ifahamike kuwa iwapo watuhumiwa hao watakutwa na hatia juu ya makosa yao, kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watalazimika kwenda jela maisha au adhabu isiyopungua miaka 30 jela.
Amber Rutty, James Delicious wafikishwa mahakamani
Reviewed by Zero Degree
on
11/02/2018 11:50:00 AM
Rating: