Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya Jumatatu Tarehe 19 Mei, 2024


Manchester United wanataka takriban asilimia 75 ya pauni milioni 75 walizolipa Borussia Dortmund kwa winga wa Uingereza Jadon Sancho, 24, ambaye atahitaji kupunguzwa mshahara wake wa pauni 275,000 kwa wiki ikiwa klabu hiyo ya Bundesliga itakamilisha dili la kumsaini tena.

Sheffield United ingelazimika kulipa kiasi cha tarakimu sita kwa kiungo wa kati wa Brazil Vinicius Souza kwa klabu ya zamani ya Lommel iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 angeanza katika mechi dhidi ya Tottenham Jumapili. (Sun)

RB Leipzig wamempa mshambuliaji wa Slovenia Benjamin Sesko mwenye umri wa miaka 20 - ambaye anahusishwa na kuhamia Arsenal - nyongeza ya muda wa kandarasi ya mwaka mmoja. (Fabrizio Romano)

Meneja wa Tottenham Ange Postecoglou ataweka kipaumbele kumsaini mshambuliaji mpya na kiungo wa safu ya ulinzi huku akipanga kuwaachilia wachezaji wengi msimu wa joto.

Bayern Munich na Ajax wanaendelea kupigania sahihi ya Erik ten Hag, 54, kwa imani kwamba atafutwa kazi kama meneja wa Manchester United mwishoni mwa msimu huu. (Mirror)

Kipa wa timu ya taifa ya Uhispania David Raya, 28, anasema hajafanya mazungumzo yoyote na Arsenal kuhusu iwapo watafanya uhamisho wake wa mkopo kutoka Brentford kuwa wa kudumu. (Express)

Ipswich wanasema wanafanya kila linalowezekana kusalia na meneja Kieran McKenna huku kukiwa na nia ya kumchukua kocha huyo kutoka kwa Brighton, Chelsea na Manchester United. (Teamtalk)


Mkufunzi wa Chelsea Mauricio Pochettino anasema atafurahi kusalia na 80-85% ya kikosi chake msimu ujao. (football.london)

Mwenyekiti mwenza wa Arsenal Josh Kroenke amewaambia mashabiki "klabu haitasimama tuli" inapotafuta wachezaji ili kusaidia kupata taji la Uingereza na Ulaya. (Goal)

West Ham wanakaribia kumsajili mlinzi mwenye umri wa miaka 18 Mwingereza Luis Brown kutoka Arsenal. (Caught Offside)
Tetesi za soka barani Ulaya Jumatatu Tarehe 19 Mei, 2024 Tetesi za soka barani Ulaya Jumatatu Tarehe 19 Mei, 2024 Reviewed by Zero Degree on 5/20/2024 11:21:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.