Loading...

Korea Kaskazini yakumbwa na mafuriko

Picha na vyombo vya habari vilionyesha Kim akisafiri ndani ya gari jeusi aina ya Lexus katika eneo lenye maji ya mafuriko

Mvua iliyovunja rekodi imesababisha maelfu ya watu kukwama kutokana na mafuriko nchini Korea Kaskazini mwishoni mwa juma, na kumfanya Kim Jong Un kutangaza "dharura", vyombo vya habari vya serikali vinaripoti.

Picha zinaonyesha mashamba na nyumba zilizozama baada ya mvua kubwa kuathiri jiji la Sinuiju na kaunti ya Uiju, ambayo inapakana na China, kulingana na Rodong Sinmun.

Kim Jon Un akisafiri katika eneo la mafuriko

Vyombo vya habari vya serikali vimesema kuwa wengi waliokolewa baadaye kwa ndege, ingawa BBC haikuweza kuthibitisha kwa uhuru maelezo ya ripoti hiyo.
Korea Kaskazini yakumbwa na mafuriko Korea Kaskazini yakumbwa na mafuriko Reviewed by Zero Degree on 7/29/2024 06:21:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.