Loading...

Dk Magufuli balaa, vitanda 300 vyatua hospitali ya taifa Muhimbili.



Rais John Magufuli      

Fedha za kununua vifaa tiba hivyo zilipatikana baada ya Rais John Magufuli kuamuru kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe za kuwapongeza wabunge, zitumike kununua vifaa tiba katika hospitali hiyo.

Dar es Salaam. Wabunge wamepongeza kitendo cha kuwasilishwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) vitanda 300, magodoro 300, viti vya magurudumu 30, blanketi 400 na mashuka 1,695 vilivyogharimu Sh251 milioni.

Fedha za kununua vifaa tiba hivyo zilipatikana baada ya Rais John Magufuli kuamuru kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe za kuwapongeza wabunge, zitumike kununua vifaa tiba katika hospitali hiyo.

Mbunge wa Mtambile (CUF), Masoud Abdallah Salum alisema uamuzi uliotolewa na Rais upo sahihi kuekeleza fedha hizo zitumike kwa mahitaji ya huduma za afya.

“Sina pingamizi kwa hilo kwa sababu ni jambo jema, lakini ni muhimu kujihakikishia kama fedha hizo zimekwenda kufanya kazi husika pasipo kufanya udanganyifu, maana kumekuwa na udhaifu sana wa matumizi sahihi ya fedha zinakoelekezwa,” alisema.

Mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba alisema kiongozi huyo ameanza kuonyesha utekelezaji wa ahadi kwa vitendo. “Kama (Rais Magufuli) anavyosema kwenye kaulimbiu yake ‘Hapa Kazi Tu’ ndiyo ameanza.

“Hata sisi (CCM) tunafurahi kwa sababu tumepata kiongozi ambaye Watanzania walikuwa wanamtaka, kiongozi wa kuwatumikia wananchi wa kada zote na vyama vyote bila kujali tofauti zao,” alisema.

Hata hivyo, Mbunge wa Chake Chake (CUF), Yussuf Kaiza Makame alisema Dk Magufuli hakutakiwa kuzipangia matumizi fedha hizo, badala yake alipaswa kulitumia Bunge liweke utaratibu wa kuzitumia.

Msemaji wa Bohari ya Dawa nchi (MSD), Ety Kusiluka alithibitisha bohari hiyo kupeleka MNH vifaa tiba vya thamani ya Sh251 milioni ambavyo vilinunuliwa na ofisi ya Bunge kwa agizo la Rais.

Alisema tayari vifaa hivyo vimepokelewa kwa ajili ya wagonjwa.


Credits: Mwananchi
Share this to all your friends.
Dk Magufuli balaa, vitanda 300 vyatua hospitali ya taifa Muhimbili. Dk Magufuli balaa, vitanda 300 vyatua hospitali ya taifa Muhimbili. Reviewed by Zero Degree on 11/23/2015 11:21:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.