Loading...

Lissu afikishwa tena mahakamani na kukutana na mashtaka matatu.

Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu.

Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu amefikisha Mahakama ya Kisutu saa 8:46 huku kukiwa na ulinzi mkali.




Ulinzi umeimarishwa mahakamani hapo muda mrefu wakati wakimsubiria Lissu akitokea katika kituo cha polisi kanda maalumu.

Polisi wapatao tisa baadhi yao wakiwa na silaha wametanda katika eneo la mbele la mahakama hiyo.



Lissu ameshtakiwa kwa makosa matatu la kwanza kutoaa maneno ya uchochezi, kwamba Agosti 2 katika Mahakama ya Kisutu kwa nia ya kujenga chuki kwa wananchi dhidi ya Rais na Serikali alitoa maneno ya uchochezi.

Shtaka la pili pia uchochezi, kwamba Agosti 2 katika mahakama hiyohiyo kwa nia ya kudharau mhimili wa utoaji haki, alisema kuwa hawezi kufungwa kwa mashtaka na kesi ya upuuzi na shtaka la tatu ni la kudharau mahakama akidaiwa kuwa tarehe hiyohiyo mahakamani hapo, alitoa maneno ya uchochezi kuwa hawezi kufungwa kwa kesi na mashtaka ambayo ni upuuzi na ya kimagufulimagufuli.


Credits: Mwananchi
ZeroDegree.
Lissu afikishwa tena mahakamani na kukutana na mashtaka matatu. Lissu afikishwa tena mahakamani na kukutana na mashtaka matatu. Reviewed by Zero Degree on 8/05/2016 09:30:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.