Loading...

Rio Ferdinand: Msimu huu Chelsea watamaliza Ligi Kuu katika nafasi hii


Rio Ferdinand ametabiri kwamba, Chelsea watamaliza Ligi katika nafasi ya tatu msimu huu.

'The Blues' tayari wameanza vibaya msimu huu wakiwa na matazamio ya kutetea ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza msimu huu baada kufanikiwa kwa Antonio Conte kutwaa taji hilo kwa namna ya kipekee msimu uliopita.

Chelsea walikuwa kwenye kiwango cha juu msimu uliopita walipofanikiwa kushinda michezo 30 ya Ligi Kuu ya Uingereza katika safari ya kuubeba ubingwa kwa mara ya pili ndani ya miaka mitatu.

Hata hivyo, vijana hao wa Antonio Conte hawakushiriki Ligi ya Mabingwa ulaya msimu uliopita na hivyo kuwafanya watazamie zaidi mashindano ya ndani.

Kwa upande wake nyota wa zamani wa Manchester United anaeleza kwamba Chelsea hawataweza kutetea taji hilo msimu huu.

Ferdinand aliandika hivi kwenye ukurasa wake wa Instagram: “Nafasi ya tatu ni ya Chelsea (hawana uwezo wa kushinda taji hilo mfululizo wakiwa na kibarua kingine
 pia kwenye Ligi ya mabingwa msimu huu).”
Rio Ferdinand: Msimu huu Chelsea watamaliza Ligi Kuu katika nafasi hii Rio Ferdinand: Msimu huu Chelsea watamaliza Ligi Kuu katika nafasi hii Reviewed by Zero Degree on 8/14/2017 02:19:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.