Loading...

Barcelona kugeukia kwa nyota huyu wa Tottenham kama watamkosa Griezman


Barcelona wamemtaja kiungo wa klabu ya Tottenham, Christian Eriksen kama mbadala wa Antoine Griezmann nayeweza pia kuwa mrithi nafasi ya Andres Iniesta.

Rais wa Atletico Madrid, Enrique Cerezo amesema kuwa Antoine Griezmann haendi kokote kwenye usajili wa majira joto.

Mfaransa huyo amekuwa akihusishiwa na uhamisho kwenda kwa Mabingwa wa La Liga, Barcelona na pia Manchester United katia siku za hivi karibuni.

Griezmann walikuwa na msimu mwingine mzuri. Alifunga mabao 29 kwenye michuano yote akiwa na vtimu hiyo inayoongozwa na Diego Simeone.

Lakini inaonekana kama vile nyota huyo wa La Liga anabaki katika klabu ya Atletico Madrid kwa msimu mwingine.

Christian Eriksen
Hivyo, Eriksen ameibuka na kuwa chaguo la kwanza kujaza nafasi hiyo lakini Barcelona hawana uhakika kama wataweza kumudu gharama za kiungo huyo wa Denmark.

Barcelona tayari wameshatumia kiasi kikubwa cha fedha kwa Phil Coutinho, ambaye bado hajafikia kiwango cha kulinganishwa na bei yake msimu huu tangu ajiunge nao akitokea Liverpool mwezi January.

Kiasi ambacho Spurs wanaweza kuhitaji ili kumruhusu raia huyo wa Denmark kinaweza kuwa kikubwa sana kiasi cha kuwakatisha tamaa vigogo hao wa Uhispania.
Barcelona kugeukia kwa nyota huyu wa Tottenham kama watamkosa Griezman Barcelona kugeukia kwa nyota huyu wa Tottenham kama watamkosa Griezman Reviewed by Zero Degree on 5/30/2018 08:50:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.