Loading...

Sababu iliyopelekea Zinedine Zidane kuondoka Real Madrid

Zinadine Zidane, shujaa wa Real Madrid kama mchezaji na kama meneja aliondoka baada ya mgogoro na rais wa klabu hiyo, Florentino Perez
Zinedine Zidane aliondoka Real Madrid baada ya mgogoro na rais wa klabu hiyo, Florentino Perez juu ya usajili.
Kwa hisia kali, Zidane anaondoka Madrid baada ya kuandika historia ya kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa mara tatu mfululizo.

Mfaransa huyo aliitisha mkutano ambao haukutarajiwa Alhamisi ya wiki iliyopita mchana kuweka wazi kwamba ataondoka baada kuitumikia klabu hiyo kwa miaka miwili na nusu.

Perez alitaka kuendelea na mkakati wa kuisaka saini ya golikipa wa Manchester United, David de Gea.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 45, shujaa wa klabu kama mchezaji na kama meneja, alisema alihisi ni muda sahihi kwa yeye kuondoka.

Kwa mujibu wa taarifa ya The Sun, usiku wa Jumatano ya wiki iliyopita Zidane na Perez walitofautiana juu ya nani ambaye anafaa kusajiliwa na klabu kwenye majira ya joto.
Zidane alikuwa na nia ya kumsajili nyota wa klabu ya Chelsea, Eden Hazard wakati Perez akitaka wakazanie saini ya golikipa wa Manchester United, David de Gea. 

Zidane alipokuwa na nia ya kumsajili nyota wa klabu ya Chelsea, Eden Hazard, rais Perez alikataa
Perez hakukubaliana na matakwa ya Zidane na baadaye pia alifurahia kuwa na golikipa wake namba moja, Keylor Navas, ambaye alitaka de Gea achukue nafasi yake.
Inadaiwa kuwa Zidane alisema: 'Nimefika mwisho. Uchukue jukumu la kuisimamia timu wewe mwenyewe' kufuatia mgogoro huo.

Aliyekuwa meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, meneja wa Tottenham, Mauricio Pochettino na aliyekuwa kiungo wa Madrid, Guti ni vinara kwenye orodha ya wagombea wa nafasi yake Bernabeu.

Akiwa pembeni ya rais Perez katika mkutano huo wiki iliyopita, Zidane alisema: 'Nimechukua uamuzi wa kutoendelea na kazi hii msimu ujao. Kwa mimi na kwa kila mtu, nafikiri wakati wa mabadiliko umefika. Haukuwa uamuzi rahisi.'

Habari nyingine kama hii:
Sababu iliyopelekea Zinedine Zidane kuondoka Real Madrid Sababu iliyopelekea Zinedine Zidane kuondoka Real Madrid Reviewed by Zero Degree on 6/05/2018 11:35:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.