Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 21 Julai, 2024

Jadon Sancho, 24

Chelsea wanaweza kuchelewa kumsajili mshambuliaji wa Manchester United na timu ya taifa ya Israel, Jadon Sancho, 24.

Manchester City wako mstari wa mbele kumsajili kiungo wa zamani wa Ujerumani Ilkay Gundogan kutoka Barcelona, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 akitanguliza kurejea Ligi Kuu ya Uingereza.

Burnley wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United na Tunisia Hannibal Mejbri, 21.

Winga wa Aston Villa Muingereza Samuel Iling-Junior mwenye umri wa miaka 20 anatafuta chaguzi za mkopo kabla ya tarehe ya mwisho ya dirisha la uhamisho. (Athletic)

Meneja wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola anatamani Gundogan arejee katika klabu hiyo. (Fabrizio Romano)

Liverpool wamewasilisha ofa iliyoboreshwa ya pauni milioni 34 kwa mlinda lango wa Valencia na Georgia Giorgi Mamadashvili, 23. (Relevo)

Manchester United wamekubali mkataba wenye thamani ya takriban £5m kwa winga wa Uruguay Facundo Pellistri, 22, kujiunga na klabu ya Ugiriki Panathinaikos.

Paris St-Germain wamewapa Manchester United nafasi ya kumsajili kiungo wa kati wa Uruguay Manuel Ugarte, 23, kwa mkopo wa msimu mmoja na jukumu la kumnunua. (Telegraph)

Barcelona hawako tayari kumsajili tena beki wa pembeni wa Manchester City na Ureno Joao Cancelo, 30, kwa sababu ya madai yake ya mshahara wa pauni milioni 12. (Sport)

Chelsea wanajiandaa kwa kibali ambacho kinaweza kuwaletea kikomo cha uhamisho wa pauni milioni 200, huku wachezaji wanane wakitarajiwa kuondoka Stamford Bridge.

Wolves na Brentford wanamtaka mchezaji wa Burnley Dara O’Shea, 25, lakini lazima walipe pauni milioni 15 ili kumsajili beki wa Jamhuri ya Ireland. (Mirror)

Eddie Nketiah, 25

Klabu ya Arsenal wanataka zaidi ya pauni milioni 30 kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Eddie Nketiah, mwenye umri wa miaka 25, baada ya kukataa dau la pauni milioni 25 kutoka kwa Nottingham Forest. (Football Insider)

Bayer Leverkusen wamewasiliana na Liverpool kuhusu uwezekano wa kumnunua Sepp van den Berg huku The Reds wakitarajiwa kuhitaji pauni milioni 25 kwa mlinzi huyo wa Uholanzi. (Florian Plettenberg)

Brentford wanatumai kupuuza juhudi za Xabi Alonso kumsajili Van den Berg kutoka klabu ya zamani ya Liverpool. (Times)

Manchester United wako tayari kumuuza kiungo wa Scotland Scott McTominay, 27, kwa Napoli ili kufuata kanuni za Financial Fair Play (FFP).

Klabu ya Barcelona wanataka kumsajili mshambuliaji wa klabu ya AC Milan na Ureno Rafael Leao kabla ya tarehe ya mwisho ya dirisha la uhamisho. (Mundo Deportivo)

Endrick, 18

Mshambulizi wa Brazil Endrick, 18, ataomba kuondoka Real Madrid kwa mkopo Januari ikiwa hatapata dakika za kutosha uwanjani mwanzoni mwa msimu. (Sport)

Manchester United haijakata tamaa ya kumsajili beki wa kati wa England Jarrad Branthwaite mwenye umri wa miaka 22 kutoka Everton, lakini wanakubali kuwa kuna uwezekano mkubwa kutokea dirisha hili la uhamisho. (Mail)

Meneja wa Manchester United Erik ten Hag amefutilia mbali mpango wa kumruhusu kiungo wa kati wa Brazil Casemiro kuondoka baada ya kufurahishwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 katika maandalizi ya msimu mpya na kuanza kwa kampeni mpya. (Sun)
Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 21 Julai, 2024 Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 21 Julai, 2024 Reviewed by Zero Degree on 8/21/2024 09:05:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.