Loading...

Kiungo wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Ze Roberto asaini mkataba mpya akiwa na umri wa miaka 42.


Inavyoonekana kwa umri wa miaka 42 ni sawa 22. Angalau hivo ndivyo waweza sema kwa Mbrazil huyo.

Kiungo wa zamani wa Real Madrid na Bayern Munich Ze Roberto amesaini mkataba mpya na klabu ya Palmeiras ya huko Brazil akiwa na umri wa miaka 42.



Wakati wake katika mpira akiwa Ulaya, Ze Roberto alishinda taji la Mabingwa barani Ulaya akiwa na klabu ya Real Madrid, huku pia akipata mataji kadhaa katika michuano mbalimbali na klabu ya Bayern, ikiwa ni pamoja na mataji manne ya ligi ya Bundesliga katika muda wake wote nchini Ujerumani.



Ze Roberto alitoa mchango mkubwa akiwa na klabu yake ya Palmeiras kwenye michuano kuwania kikombe cha Campeonato Brasileiro mwaka 2016 na ameshaonekana katika mechi 53 kwa klabu yaake hiyo tangu ajiunge nayo mwaka 2015.

"Motisha yangu kubwa daima imekuwa kutenda kazi. Malengo yamefanikiwa - kushinda taji la 'Copa do Brasil' mwaka jana na sasa taji jingine la Brasileirão, "
 alisema Ze Roberto.


"Nilipofika kwa mara ya kwanza, nilisema kwamba sikuja kusogeza muda tu, lakini nimekuja ili kuwa sehemu ya historia ya klabu hii, kuona picha yangu katika chumba cha kubadilishia nguo. Hilo limetimia na nina furaha sana."



Nyota huyo mwenye umri wa miaka 42 alikuwa na mafanikio miaka 12 ya kazi ya kimataifa na timu yake ya taifa Brazil kuanzia 1995 hadi 2006, ambayo ni pamoja na mabao sita katika mechi 84 kwa mabingwa mara tano wa Kombe la Dunia. Pamoja na timu ya taifa, Ze Roberto ameshikilia mataji mawili ya Copa America kwa Brazil mwaka 1997 na 2005.

ZeroDegree.
Kiungo wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Ze Roberto asaini mkataba mpya akiwa na umri wa miaka 42. Kiungo wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Ze Roberto asaini mkataba mpya akiwa na umri wa miaka 42. Reviewed by Zero Degree on 12/10/2016 11:35:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.