Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano ya Tarehe 20 Septemba, 2017


Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho ana matumaini ya kumsajili mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez mbele ya mahasimu wao wa jijini, Manchester City katika majira ya joto mwakani.

Hofu ya Manchester United kumpoteza David de Gea kwa Real Madrid inaweza kupungua sasa baada ya Zinedine Zidane kuonesha nia ya kutaka kumsajili Goli kipa wa Athletic Bilbao (Spain U21), Kepa.


Liverpool wanaweza kumpoteza Emre Can ambaye anaweza kuondoka kama mchezaji huru kwa sababu hawako tayari kumuachia kiungo huyo aondoke. (Chanzo: The Sun)

Inter Milan wamemshawishi Ivan Perisic aachane na mawazo ya kuelekea Man Utd na hawajaonesha nia ya kumwacha aondoke.

Manchester City wameanza mazungumzo na mshambuliaji wao kBrazili, Gabriel Jesus kuhusiana na mkataba mpya kabla hajatimiza miezi 10 akiwa amejiunga na klabu hiyo.

Ronald Koeman (Everton) amewaambia wachezaji wake kurudisha fikra zao pamoja ili kukabiliana vyema na wapinzani uwanjani. (Chanzo: The Star)

Arsene Wenger ameonyesha nia ya wazi kumpa Jack Wilshere mkataba mpya kama ataongeza bidii ya mchezo kwa kusema kwamba anahisi itakuwa ni ndoto ya kiungo huyo kuendelea kubakia Arsenal. (
Chanzo: Daily Telegraph)

Manchester United watasimamia maneno yanayoimbwa kwenye nyimbo za mashabiki kwenye michuano ya Carabao dhidi ya Burton Albion leo Jumatano usiku baada ya wimbo unaomhusu Romelu Lukaku kulalamikiwa kuwa ni wa kibaguzi.

Wayne Rooney amemuacha Ronald Koeman njia panda kwenye suala la kupanga kikosi kwa kuomba kuanza kikosi cha kwanza kwenye mchezo wa Carabao kati ya Everton na Sunderland. (Chanzo: Daily Mail)

Tony Pulis anadai Jonny Evans ana thamani ya paundi milioni 30 kiasi ambacho Manchester City were hawakuwa tayari kutoa. (Chanzo: Daily Mirror)


Antonio Conte amempa nafasi Ethan Ampadu, kinda aliyesajiliwa kutoka Exeter City katika majira ya joto, kwenye kikosi kitakachoivaa Nottingham Forest kwenye michuano ya Carabao, ambapo Chelsea wanategemewa kufanya mabadiliko makubwa ya wachezaji katika mchezo huo unaochezewa Stamford Bridge. (Chanzo: The Gurdian)

Real Madrid wanaweza kumuuza Karim Benzema kwa Arsenal kufanikisha uhamisho wa Alexis Sanchez. (Chanzo: Daily Express)
Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano ya Tarehe 20 Septemba, 2017 Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano ya Tarehe 20 Septemba, 2017 Reviewed by Zero Degree on 9/20/2017 05:49:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.