Loading...

Museveni ashtakiwa mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai [ICC]

Rais Museveni wa Uganda
Wabunge wanne wa chama cha upinzani nchini Uganda cha Forum for Democratic Change- FDC- kutoka maeneo ya magharibi mwa Uganda huko Kasese, wamemshtaki kiongozi wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni, katika mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai -ICC, iliyoko The Hague nchini Uholanzi.

Wanasiasa hao wanamhusisha katika kile wanachokiita mauaji mabaya wakati vikosi vya usalama vilipovamia kasri la mfalme wa Rwenzururu Wesley Mumbere.

Wabunge hao chini ya kiongozi wa upinzani bungeni na mbunge wa FDC wa Kasese Winnie Kizza, wameyasema hayo leo mjini Kampala, walipokuwa wakiwahutubia waandishi wa habari.

ZeroDegree.
Museveni ashtakiwa mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai [ICC] Museveni ashtakiwa mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai [ICC] Reviewed by Zero Degree on 1/05/2017 09:22:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.